TANGAZO WANAWAKE:SABABU KUMI KWAMBA MPENZI WAKO NI “MWANAUME” SIO “MVULANA”
Sunday 13, Apr 2025

WANAWAKE:SABABU KUMI KWAMBA MPENZI WAKO NI “MWANAUME” SIO “MVULANA”

men+and+black+suit.jpg+4
1.Anapoishi, Pana Muonekano wa “Nyumbani” sio “Nyumba” yaani sio lazima awe na mali nyingi, wala si lazima iwe nyumba yake. Jambo la msingi ni je, anajali makazi yake? Hata kama anaishi chumba kimoja, je, sakafu ya nyumba ina rangi yake ya asili?

2.Ana Malengo ya Maisha na Kufanya anachokipenda bila kujali anakutana na changamoto gani. Mwanaume mwenye ukomavu kiakili siku zote anamipango ya kutoka hatua A kwenda B na kuna kitu cha ndani kinachomvuta afanye hivyo.


3.Anauwezo wa kujitegemea kimaisha, na yeye mwenyewe kiujumla. Yaani  hata kama amelewa hategemei mtu ampeleke nyumbani.

4.Ana Msimamo na mipaka yake, Si kila utakachomuambia anakubaliana nacho.

5.Siku zote anajua anataka nini, vipaumbele vyake maishani, na wewe ni mmoja wa vipaumbele hivyo. La sivyo unaishi na Mvulana si MwanaUme

6.Hakuambii Huwezi siku zote, Mwanaume wa kweli anakupa moyo, na anamuda wa Kukusaidia kutimiza ndoto zako, anajua mahitaji ya mpenzi wake na kuyatengea Muda Fulani.

7.Hufanya Maamuzi, japo haoni tatizo kukuacha ufanye baadhi ya maamuzi pia.

8.Anajua Thamani yako, Hakuambii tu anakupenda, bali hukuonyesha ni jinsi gani anakupenda.

9.Hakuonei aibu.


10. Anajipenda, anajituma, Anavaa na kufanya mambo kiutu uzima na ana malengo yake ya baadae.

0 comments:

Post a Comment

Toa maoni yako

Copyright © 2014 Kumi Muhimu