KILA MTU HUFANYA UJINGA HUU IKIWEMO WEWE HASA UKIWA UMECHOKA! (KUMI)
1.Kuingia kwenye chumba halafu ghafla unasahau uliingia
kufanya nini, ukiamua kutoka tu, unakumbuka!
2.Kuangalia saa na baada ya kuondoa macho tu kwenye saa,
unasahau ilikuwa saa ngapi! Na inakubidi uangalie tena!
3.Kukubaliana na mtu kwa kutikisa kichwa kumbe hata
hujasikia kakuambia nini. Unaombea tu asije akawa amekuuliza swali
4.Unatembea katikati ya watu mara ghafla unagundua umekosea
njia, Unajidai umesahau kitu au kuangalia simu yako na kuanza kurudi kwa kasi!
5.Unabishana kichwani kwako mwenyewe mpaka unapata hasira,
baadae unagundua ni mawazo tu na kujiona
mjinga!
6. Betri za rimoti yako zimekwisha unaamua kuminya batani za rimoti kwa nguvu zaidi ukihisi itasaidia!
7.Unaambiwa kitu Fulani ni cha moto, unaamua kugusa na
unaungua kweli!
8. Unajikwaa au kujigonga sehemu na unaanza kutukana ukihisi sehemu hiyo inakusikia
9 Kujiangalia kwenye kioo cha jengo na kusahau kuwa kuna
watu ndani ya jengo na wanakuagalia
10. Unabisha kwamba hujalala (huko usingizini) na unasikia
kila kinachoongelewa, kumbe kila mtu ameshakushtukia!
0 comments:
Post a Comment
Toa maoni yako